Breaking News

RC Gambo amewataka wananchi kuwafichua wanaokwepa kod


Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ameitaka mamlaka ya mapato kushirikiana na wananchi kuwafichua wanaokwepa kulipa kodi.
Gambo ameyasema hayo wakati akizungumza katika wiki ya Elimu kwa mlipa kodi iliyoenda sambamba na utoaji elimu kuhusu ulipaji kodi na faida zake.
Amesema kuwa wananchi wana taarifa nyingi juu ya watu wachache ambao sio waadilifu katika suala la kulipa kodi hivyo ameitaka tra kushirikiana nao ili kuwafichua.
Mmoja wa wafanyabiashara Abduly Bale wanaomiliki mgahawa awashauri mamlaka ya mapato kuwaangalia wafanya biashara wadogo wadogo ambao huathiri wao kibiashara kwa kua hawana leseni wala kulipia mapato  na wao  hulipia leseni pamoja na mapato .
Mwenyekiti wa chama cha Madalali wa Madini Arusha Jeremia Simoni ameiomba mamlaka ya mapato kuwaangalia tajiri mwenye mali na mnunuzi ndio wanaotakiwa kulipia mapato kwani wao hufanya biashara bila mtaji.
Meneja TRA mkoa wa Arusha  Faustin Mdesa  amesema mamlaka ya mapato imekua na malengo ya kusisitiza utoaji wa risiti katika mauzo ya wafanya biashara mfumo huo utawatunzia hesabu zao kua na uhakika wa mauzo  yao.
Faustin amesema kuwa ulipaji kodi unapaswa kuwa utamaduni wa kila mtanzania ili kuachana na kasumba ya kukwepa kodi inayorudisha nyuma maendeleo ya nchi.

No comments