Mkurugenzi wa facebook aitwa kwa barua rasmi na kamati ya Bunge
Cambridge Analytica ni kampuni ambayo iko nchini Uingereza ambayo inatuhumiwa kutumia taarifa za wanachama Milioni 50 ili kuweka ushawishi katika Uchaguzi Mkuu wa Urais nchini Marekani uliofanyika mwaka 2016.
Kampuni ya Facebook inatuhumiwa kwa kosa la kushindwa kuwapa taarifa watumiaji wa mtandao huo kuwa, taarifa zao zinaweza kuwa zilipatikana na kutunzwa na kampuni hiyo ya Cambridge Analytica, kampuni ambayo inasemekana kumsaidia Donald Trump kushinda Urais 2016 Marekani.
Hatahivyo Facebook imeeleza kuwa iliifungia kampuni hiyo kupata taarifa za mtandao huo, japokuwa iliweza kupata taarifa hizo kwa njia za udanganyifu na kuvunja sera za mtandao huo.
No comments