Azam uso kwa uso na Mbao leo
Klabu Bingwa Afrika Mashariki na kati AzamFc kuvaana na MbaoFC ya
Jijini Mwanza baada ya kumalizana na Mwadui FC ambapo wanalambalamba
hao walitoka kifua mbele kwa kuifunga timu hiyo bao 1-0 katika uwanja wa
Azam Complex Chamazi.
Timu hizo mbili zitapimana nguvu hapo kesho majira ya saa1 Usiku katika dimba la Uwanja Wa Azam Complex Chamazi. Ambapo kila timu zina presha ya kutaka kupata ushindi wa kuibuka na Alama 3 ili kuweza kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi.
Akizungumza na waandishi Wa Habari Ofisa Habari AzamFc Jaffary Iddy leo katika ofisi zao Mzizima Jijini Dar es salaam amesema kuwa kikosi tayari kipo kambini na kinaendelea na mazoezi.
"Kikosi kipo kambini kinaendelea na mazoezi yake katika kuelekea kwenye mchezo huo wa aina yake Ambapo kila timu inaitaji ushidi, tunaieshimu Timu ya Mbao iko vizuri na Ina kikosi kizuri lakini na sisi Tumejipanga vema kubakiza Alama 3 Nyumbani"amesema msemaji huyo Jaffary.
Maganga amesema kuwa wataendelea kumkosa mchezaji wao Yakubu Mohammed ambaye alipata majeraha pamoja na Kipa wao namba 1 Razack Abarola.
"Wachezaji Wote wako fiti ila tutaendelea kumkosa mchezaji wetu Yakubu Mohammed aliyepata majeraha katika mchezo wa michuano ya kombe la shirikisho FA Cup ambapo tulicheza na timu ya KMC pamoja na kipa wetu Razack Abarola anaemalizia kutumikia adhabu ya kutoshiriki Mechi tatu" amesema Jaffary Maganga.
Timu hizo mbili zitapimana nguvu hapo kesho majira ya saa1 Usiku katika dimba la Uwanja Wa Azam Complex Chamazi. Ambapo kila timu zina presha ya kutaka kupata ushindi wa kuibuka na Alama 3 ili kuweza kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi.
Akizungumza na waandishi Wa Habari Ofisa Habari AzamFc Jaffary Iddy leo katika ofisi zao Mzizima Jijini Dar es salaam amesema kuwa kikosi tayari kipo kambini na kinaendelea na mazoezi.
"Kikosi kipo kambini kinaendelea na mazoezi yake katika kuelekea kwenye mchezo huo wa aina yake Ambapo kila timu inaitaji ushidi, tunaieshimu Timu ya Mbao iko vizuri na Ina kikosi kizuri lakini na sisi Tumejipanga vema kubakiza Alama 3 Nyumbani"amesema msemaji huyo Jaffary.
Maganga amesema kuwa wataendelea kumkosa mchezaji wao Yakubu Mohammed ambaye alipata majeraha pamoja na Kipa wao namba 1 Razack Abarola.
"Wachezaji Wote wako fiti ila tutaendelea kumkosa mchezaji wetu Yakubu Mohammed aliyepata majeraha katika mchezo wa michuano ya kombe la shirikisho FA Cup ambapo tulicheza na timu ya KMC pamoja na kipa wetu Razack Abarola anaemalizia kutumikia adhabu ya kutoshiriki Mechi tatu" amesema Jaffary Maganga.
No comments